Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mufalme Ahasuero akawaambia malkia Esteri na Mordekayi, yule Muyuda: “Muangalie! Nimemupa Esteri mali ya Hamani, naye wamekwisha kumutundika kwa sababu ya shauri lake baya juu ya Wayuda.

Gade chapit la Kopi




Esteri 8:7
7 Referans Kwoze  

Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.


Kwa mwanzo wa utawala wa mufalme Ahasuero, waadui za watu waliokaa Yuda na Yerusalema wakaandika mashitaki juu yao.


Siku ileile, mufalme Ahasuero akamupatia malkia Esteri mali yote ya Hamani, adui ya Wayuda. Esteri akamujulisha mufalme kwamba Mordekayi ni ndugu yake. Basi, tangu wakati ule, Mordekayi akaruhusiwa kumwona mufalme.


Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite