Basi, Hamani akatwaa nguo zile na kumuvalisha Mordekayi, akamutembeza kwenye kiwanja cha muji akiwa juu ya farasi wa mufalme, naye akitangaza: “Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.”
na mumoja wa washauri wako wa kuheshimika ee mufalme amuvalishe mutu yule nguo hizo za kifalme, na kumwongoza mutu yule akiwa amepanda juu ya farasi wako mpaka kwenye kiwanja cha muji, naye akitangaza: ‘Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.’ ”
Hamani alipoingia ndani, mufalme akamwuliza: “Nimufanyie nini mutu ambaye ningependa sana kumupatia heshima?” Hamani akafikiri ndani ya moyo wake: “Ni nani huyo ambaye mufalme angependa kumupatia sana heshima? Bila shaka ni mimi.”