Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hamani alipoingia ndani, mufalme akamwuliza: “Nimufanyie nini mutu ambaye ningependa sana kumupatia heshima?” Hamani akafikiri ndani ya moyo wake: “Ni nani huyo ambaye mufalme angependa kumupatia sana heshima? Bila shaka ni mimi.”

Gade chapit la Kopi




Esteri 6:6
19 Referans Kwoze  

Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Lakini wanaotaka kuona kwamba sina kosa, wakuwe na furaha tele, waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa! Anapendezwa na kumupatia mutumishi wake uheri.”


Basi, Hamani akatwaa nguo zile na kumuvalisha Mordekayi, akamutembeza kwenye kiwanja cha muji akiwa juu ya farasi wa mufalme, naye akitangaza: “Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.”


na mumoja wa washauri wako wa kuheshimika ee mufalme amuvalishe mutu yule nguo hizo za kifalme, na kumwongoza mutu yule akiwa amepanda juu ya farasi wako mpaka kwenye kiwanja cha muji, naye akitangaza: ‘Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.’ ”


Basi, Hamani akamujibu mufalme: “Mutu huyo ambaye mufalme angependa kumupatia heshima,


Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Basi, watumishi wakamujibu mufalme: “Hamani yuko katika kiwanja.” Mufalme akasema: “Mumukaribishe ndani.”


Akawauliza hivi: “Kulingana na sheria, malkia Vashiti afanyiwe nini? Maana, nimewatuma matowashi wangu kwake, lakini yeye amekataa kuitii amri yangu, mimi mufalme Ahasuero!”


Naye anapokuja, yule aliyewaalika ninyi wawili, ataweza kuja kukuambia: ‘Umwachie mutu huyu kiti.’ Halafu utapatwa na haya kwenda kuikaa kwenye viti vya nyuma.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite