Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kule akawaelezea Zeresi, muke wake, na warafiki zake wote mambo yote yaliyomupata. Zeresi na hao warafiki zake wakamwambia: “Ikiwa huyu Mordekayi, ambaye umeanza kupoteza madaraka yako kwa ajili yake ni wa kabila la Wayuda, basi, hautamuweza; atakushinda kabisa.”

Gade chapit la Kopi




Esteri 6:13
16 Referans Kwoze  

Mwenye mwenendo mukamilifu ataponyeshwa, lakini munafiki wa njia mbili ataanguka mara moja.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.


Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo, atainua kichwa chako kusudi akutundike juu ya muti, nao ndege watakula mwili wako.”


Kusikia hivyo, mufalme Nebukadneza alikasirika na kuwa na hasira sana, akaamuru wenye hekima wote wa Babeli waangamizwe.


Mambo kama yale nimeyasikia mengi; ninyi ni wafariji wenye kutaabisha!


Taabu na uchungu, vinamutisha; vinamushambulia kama jeshi la mufalme anayekuwa tayari kwa vita


Yule mutumishi akamwelezea Isaka yote aliyokuwa ameyafanya.


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.


“Musiwaguse wachaguliwa wangu; musiwazuru manabii wangu!”


Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite