Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hamani akatoka kule kwenye karamu mwenye furaha tele na moyo mukunjufu. Lakini alipomwona Mordekayi kwenye mulango wa nyumba ya kifalme, hasimami wala hamupi heshima, Hamani akawaka hasira.

Gade chapit la Kopi




Esteri 5:9
19 Referans Kwoze  

Hamani akawaka hasira alipojua kwamba Mordekayi hainami wala kupiga magoti mbele yake.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Musikitike, mulie na kulalamika. Kucheka kwenu kugeuke kuwa kilio, na furaha yenu igeuke kuwa huzuni.


Kweli, kweli ninawaambia: mutalia na kusikitika, lakini watu wa dunia watafurahi. Mutahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.


Ole kwenu ninyi munaoshiba sasa, maana mutasikia njaa. Ole kwenu ninyi munaocheka sasa, maana mutahuzunika na kulia.


Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.


Hata jeshi likinizunguka, moyo wangu hautaogopa kitu; hata nikishambuliwa kwa vita, sitakata tumaini.


Watumishi wangu wote wanasema wazi, kila mugeni amekaribishwa katika nyumba yangu.


mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!


Mufalme akaamuru wakubwa wote wa serikali yake wamutii Hamani kwa kuinama na kupiga magoti mbele yake. Lakini Mordekayi hakuinama wala kupiga magoti mbele yake.


Wabinti walipokusanyika mara ya pili, Mordekayi alikuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme.


Hapo, Ahabu akarudi kwake akijaa chuki na huzuni nyingi, kwa sababu Naboti wa Yezereheli alimwambia kwamba hatamupa kile alichorizi kutoka kwa wazee wake. Basi, akalala kwenye kitanda, akaficha uso wake na kukataa chakula.


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Lakini yote haya hayanifalii kitu ikiwa nitaendelea kumwona yule Muyuda Mordekayi kwenye mulango wa nyumba ya kifalme.”


Naye akamwambia: “Kwa sababu nilizungumuza na Naboti wa Yezereheli, nikataka aniuzishie shamba lake la mizabibu, au kama akipenda nimupe shamba lingine pahali pa lile. Lakini yeye akaniambia: ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite