Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya mambo hayo, mufalme Ahasuero akamupandisha Hamani cheo, akakuwa waziri mukubwa. Hamani alikuwa mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.

Gade chapit la Kopi




Esteri 3:1
15 Referans Kwoze  

Watakuwa na hazina ya kutosha ya maji, mbegu yao itapata maji mengi, mufalme wao atakuwa mukubwa kuliko Agagi, na ufalme wake utatukuka sana.


Mufalme Dario aliamua kuweka wakubwa mia moja na makumi mbili kwa kusimamia mambo ya ufalme.


Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.


Mufalme akaivua pete yake, ambayo ilitumiwa kwa kupiga muhuri juu ya matangazo, akamupa adui wa Wayuda Hamani mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.


Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.


Wewe ndiwe utakayeisimamia inchi yangu, na watu wangu wote watakuwa chini ya amri yako. Mimi tu ndiye mukubwa kuliko wewe kwa kuwa ninaikalia kiti cha kifalme.


Wenye haki wakiongozeka, watu wanafurahi. Lakini waovu wakitawala, watu wanalalamika.


Utulinde, ee Yawe, utukinge siku zote na kizazi hiki kiovu.


Kisha Esteri akazungumuza tena na mufalme; akajitupa chini, kwenye miguu ya mufalme, naye akilia, akamusihi mufalme aukomeshe mupango mubaya ambao Hamani, wa uzao wa Agagi, alikuwa amepanga juu ya Wayuda.


Esteri akamujibu: “Adui yetu mukubwa na mutesaji wetu, ni huyu mwovu Hamani!” Hapo Hamani akashikwa na hofu mbele ya malkia na mufalme.


Washauri wake wa kawaida walikuwa Karsena, Setari, Adimata, Tarsisi, Maresi, Marsena na Memukani – viongozi saba wa Persia na Media waliokuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.


Mimi pamoja na washauri wangu saba, tunakutuma uende ufanye uchunguzi kule Yuda na Yerusalema kuona kama Sheria ya Mungu wako ambayo umepewa inafuatwa kikamilifu.


Alimukamata mateka mufalme Agagi wa Waamaleki akiwa angali muzima. Akawaua watu kwa makali ya upanga.


Wakati wanainchi wa Misri walipoanza kuona njaa, wakamulilia mufalme awape chakula. Naye akawaambia Wamisri wote: “Mwende kwa Yosefu; mufanye neno lolote atakalowaambia.”


wapumbafu wanapewa kazi za madaraka ya juu, na watajiri wanakamata nafasi za mwisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite