Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hegayi akapendezwa na Esteri hata kiasi cha kumupendelea. Bila kupoteza wakati, akamupa Esteri mafuta na chakula. Vilevile, akamuhamishia pahali pazuri kabisa katika nyumba hiyo ya wanawake, akamuchagulia wajakazi saba kutoka nyumba ya mufalme.

Gade chapit la Kopi




Esteri 2:9
12 Referans Kwoze  

Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.


Kipindi cha hao wabinti kwa kujipodoa na kujitia uzuri kilikuwa mwaka mumoja: miezi sita ya kwanza walitumia mafuta ya manemane, na miezi sita ya mwisho walitumia marasi na mafuta mengine. Nyuma ya pale, kila binti, peke yake, alipelekwa kwa mufalme Ahasuero.


Mufalme achague wakubwa katika kila jimbo la utawala wake, na kuwaagiza wawalete wabinti wote wazuri ambao ni mabikira kwenye nyumba ya wanawake hapa Susani, muji mukubwa. Halafu wawekwe chini ya uangalizi wa Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wako; na hapo wapewe mafuta na vifaa vingine kusudi wajipambe zaidi.


Basi, Mungu akamujalia Danieli kupendelewa na kuhurumiwa na Aspenazi, yule mukubwa.


Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Aliwafanya wale waliowaangamiza wawaonee huruma.


Uwasamehe watu wako zambi walizotenda mbele yako na uasi wao, uwahurumie mbele ya waadui zao, kusudi nao wapate kuwahurumia,


Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.


Mufalme alipomwona malkia Esteri akisimama katika kiwanja, Esteri akapata kukubaliwa mbele yake, naye akamunyooshea fimbo ya zahabu aliyokuwa akishika katika mukono wake. Esteri akakaribia, akagusa incha ya fimbo.


Basi, Yosefu akapata kukubaliwa mbele ya Potifari, hata akakuwa mutumishi wake wa pekee. Akamufanya musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite