Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Mufalme akamupenda zaidi Esteri kuliko wanawake wote. Naye Esteri akapata kukubaliwa na kutendewa mema mbele yake zaidi kuliko wabinti wengine wote. Basi, mufalme akamuvalisha taji ya kimalkia kwenye kichwa, akamufanya malkia pahali pa Vashiti.

Gade chapit la Kopi




Esteri 2:17
10 Referans Kwoze  

Halafu miti yote katika inchi itajua kwamba mimi Yawe ninaishusha miti mirefu na kuinua miti mifupi. Mimi ninakausha miti mibichi na kustawisha miti yenye kukauka. Ni mimi Yawe ninayesema hayo na nitayafanya.


Ukikaa kimya wakati kama huu, musaada utawafikia Wayuda kutoka pahali pengine, nao wataokolewa; lakini wewe utakufa, na jamaa ya baba yako itaangamia. Ni nani anayejua pengine umefanywa kuwa malkia kwa ajili ya wakati kama huu!”


Akawaamuru hao wamuletee malkia Vashiti, akiwa amevaa taji yake ya kimalkia. Malkia yule alikuwa na sura nzuri sana, hivyo mufalme alitaka kuwaonyesha wageni wake na viongozi uzuri wake.


Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.


Basi, Esteri akapelekwa katika nyumba kwa mufalme katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Ahasuero, mwezi wa kumi unaoitwa Tebeti.


inafaa watumishi wa mufalme walete nguo safi ya kitani mufalme aliyovaa na farasi wake mwenyewe,


Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite