Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 2:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Wakati ukafika wa Esteri kwenda kwa mufalme. Huyo, binti wa marehemu Abihaili, binamu ya Mordekayi, na ambaye alilelewa na Mordekayi, hakuomba kitu chochote zaidi ya kile alichopangiwa na Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wa mufalme. Esteri akapata kukubaliwa mbele ya kila mutu aliyemwona.

Gade chapit la Kopi




Esteri 2:15
10 Referans Kwoze  

Hakuna anayekuwa sawa njiwa yangu. Anaenea kabisa. Ni kipenzi cha mama yake, ni binti wake pekee. Wabinti wanamwangalia na kumwita mwenye heri, nao malkia na wahabara wanaimba sifa zake.


Mufalme achague wakubwa katika kila jimbo la utawala wake, na kuwaagiza wawalete wabinti wote wazuri ambao ni mabikira kwenye nyumba ya wanawake hapa Susani, muji mukubwa. Halafu wawekwe chini ya uangalizi wa Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wako; na hapo wapewe mafuta na vifaa vingine kusudi wajipambe zaidi.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Halafu malkia Esteri, binti ya Abihaili, akaandika barua kwa mamlaka yake yote, pamoja na Mordekayi Muyuda kuhakikisha ile Mordekayi aliyoiandika pale mbele juu ya Purimu.


Mimi nilikuwa ukuta, na maziba yangu kama minara yake. Mbele yake nilikuwa kama mwenye kupata amani.


Magaribi ulikuwa ndio wakati wa kwenda, na kesho yake asubui, binti huyo alipelekwa katika nyumba nyingine ya wanawake, chini ya uongozi wa Sasagazi, towashi musimamizi wa wahabara wa mufalme. Binti hakupaswa kurudi kwa mufalme, isipokuwa kama mufalme amependezwa naye, na aliitwa kwa jina.


Basi, Esteri akapelekwa katika nyumba kwa mufalme katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Ahasuero, mwezi wa kumi unaoitwa Tebeti.


Siku ileile, mufalme Ahasuero akamupatia malkia Esteri mali yote ya Hamani, adui ya Wayuda. Esteri akamujulisha mufalme kwamba Mordekayi ni ndugu yake. Basi, tangu wakati ule, Mordekayi akaruhusiwa kumwona mufalme.


Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite