Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kipindi cha hao wabinti kwa kujipodoa na kujitia uzuri kilikuwa mwaka mumoja: miezi sita ya kwanza walitumia mafuta ya manemane, na miezi sita ya mwisho walitumia marasi na mafuta mengine. Nyuma ya pale, kila binti, peke yake, alipelekwa kwa mufalme Ahasuero.

Gade chapit la Kopi




Esteri 2:12
10 Referans Kwoze  

Munajipakaa marasi na mafuta kwa wingi kisha munakwenda kumwabudu Moleki. Munawatuma wajumbe wenu huko na huko, kujitafutia miungu ya kuabudu; hata kuzimu walifika.


Nimekinyuzia marasi, manemane, udi na mudalasini.


Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa kama munara wa moshi, kinachotoa harufu ya manemane na ubani, manukato yanayouzishwa na wachuuzi?


Mufalme achague wakubwa katika kila jimbo la utawala wake, na kuwaagiza wawalete wabinti wote wazuri ambao ni mabikira kwenye nyumba ya wanawake hapa Susani, muji mukubwa. Halafu wawekwe chini ya uangalizi wa Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wako; na hapo wapewe mafuta na vifaa vingine kusudi wajipambe zaidi.


Hegayi akapendezwa na Esteri hata kiasi cha kumupendelea. Bila kupoteza wakati, akamupa Esteri mafuta na chakula. Vilevile, akamuhamishia pahali pazuri kabisa katika nyumba hiyo ya wanawake, akamuchagulia wajakazi saba kutoka nyumba ya mufalme.


Kila siku Mordekayi alipitapita mbele ya kiwanja cha nyumba hiyo ya wanawake kusudi apate kujua hali ya Esteri na mambo ambayo yangemupata.


Wakati wa kwenda kwa mufalme, kila binti alipewa kila kitu alichotaka kutwaa kutoka nyumba ya wanawake kwenda nacho katika nyumba ya kifalme.


Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite