Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.

Gade chapit la Kopi




Esteri 1:3
16 Referans Kwoze  

Siku moja Herodia alipata wakati wa kumwua Yoane. Ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, wakati alipofanya karamu kwa wasimamizi wa serikali yake, wakubwa wa waaskari na waheshimiwa wa Galilaya.


Siku moja mufalme Belsasari alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakubwa wake na kunywa divai pamoja nao.


Kisha mufalme akafanya karamu kubwa kwa heshima ya Esteri, akawaalika viongozi na watumishi wote wa serikali yake. Vilevile, mufalme akatangaza musamaha wa kodi katika majimbo yote, akatoa zawadi nyingi kulingana na mapato yake ya kifalme.


Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.


Yule kondoo dume uliyemwona mwenye pembe mbili, ni wafalme wa Media na Persia.


Naye mufalme Dario, wa inchi ya Wamedi, akatwaa utawala akiwa na umri wa miaka makumi sita na miwili.


PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.


Washauri wake wa kawaida walikuwa Karsena, Setari, Adimata, Tarsisi, Maresi, Marsena na Memukani – viongozi saba wa Persia na Media waliokuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Basi, kwa muda wa miezi sita, Ahasuero akaonyesha utajiri wa ufalme wake mutukufu, na sifa ya utawala wake.


Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza unaoitwa Nisani, wakapiga Purimu, maana yake kura, mbele ya Hamani kusudi ajue mwezi na siku ya kuwaangamiza. Basi kura ikaangukia mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite