Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuwa na hasira kwa ajili ya muji wako Yerusalema, mulima wako mutakatifu. Watu wote wa inchi za jirani wanauzarau Yerusalema na watu wako, kwa sababu ya zambi zetu na maovu babu zetu waliyotenda.

Gade chapit la Kopi




Danieli 9:16
33 Referans Kwoze  

Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Basi, nilipokuwa nikiomba, nikiitikia zambi zangu na zambi za watu wangu wa inchi ya Israeli, pamoja na kumusihi Yawe kwa ajili ya mulima wake mutakatifu,


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Kwa haki yako uniokoe na kunikomboa; unitegee sikio lako na kuniokoa!


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Lakini tukiitikia zambi zetu mbele ya Mungu, yeye atatusamehe zambi zetu na kutusafisha toka katika maovu yote kwa maana yeye ni mwaminifu na mwenye haki.


Kwa maana, Mungu yuko na haki ya kuwatesa wale wanaowatesa ninyi,


Tena, wewe Yerusalema nitakufanya kuwa ukiwa na kitu cha kuchekelewa kati ya mataifa yanayokuzunguka na mbele ya watu wote wanaopita karibu nawe.


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Zaburi ya Daudi. Usikie maombi yangu, ee Yawe! Ulitegee ombi langu sikio, maana wewe ni mwaminifu; unijibu kwa sababu ya haki yako.


Wewe unaniimarisha katika ukamilifu; utanichunga mbele yako milele.


Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.


Yawe anawafanya wamoja wakuwe wamasikini, na wengine wakuwe watajiri. Anawashusha wamoja, na kuwainua wengine.


Umezuia kasirani yako yote; umeacha hasira yako kali.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Muji huu umechochea hasira yangu na kuniuzi tangu siku ulipojengwa mpaka leo hii. Kwa hiyo, nitauondoa kabisa mbele yangu,


Zaidi ya hayo, atapiga mahema yake makubwa kati ya bahari na mulima mutukufu na mutakatifu. Lakini atakuwa amefikia ukomo wake, na hakutakuwa mutu yeyote wa kumusaidia.


Ee Bwana, ukumbuke matusi ya mutumishi wako, jinsi ninavyovumilia mazarau ya mataifa.


Una makosa kutokana na damu uliyomwanga. Umejichafua kwa sanamu ulizojifanyia. Umeileta siku yako ya azabu karibu nawe; siku zako zimehesabiwa. Ndiyo maana nimekufanya uchekelewe na mataifa na kuzarauliwa na inchi zote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite