Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Alipokuwa anazungumuza nami, mimi nikashikwa na usingizi muzito nikiwa nimelala uso mpaka chini. Lakini yeye akanishika na kunisimamisha.

Gade chapit la Kopi




Danieli 8:18
13 Referans Kwoze  

Yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa kwa mara ingine, akanitia nguvu.


Kwa wakati ule Petro na wenzake walikuwa wamewezwa sana na usingizi; lakini wakaamuka, wakaona ule utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wakisimama pamoja naye.


Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.


Alipokuwa akisema nami, Roho wa Mungu akaniingia na kunisimamisha wima. Halafu nikamusikia


Na sasa ninasimama hapa kuhukumiwa kwa sababu ninatumainia ile ahadi Mungu aliyotoa kwa babu zetu.


Kisha kuomba, alirudia pahali alipoacha wanafunzi wake, akawakuta wamelala kwa sababu walikuwa na huzuni.


Yule malaika aliyeongea nami, akanifikia tena, akaniamusha kama vile kumwamusha mutu toka katika usingizi.


Mimi Danieli, nikazimia na kuugua kwa muda. Nilipopona, nikaendelea na shuguli za mufalme. Lakini yale maono yalishangaza, nami sikuweza kuyaelewa.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto, wakati usingizi muzito unawashika watu.


Jua lilipokuwa likitua, Abramu akashikwa na usingizi muzito. Hofu na giza nene vikamufunika.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite