Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.

Gade chapit la Kopi




Danieli 8:17
27 Referans Kwoze  

Kisha akaniambia: Sikiliza, ninakufahamisha jinsi matokeo ya kasirani ya Mungu yatakavyokuwa. Maono hayo yanaelekea wakati wa mwisho.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Lakini wewe, ee Danieli, ujiendee, upumzike katika kaburi, na wakati huo utakapotimia, utafufuka na kupata zawadi yako.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Ni mimi Yoane niliyesikia na kuona mambo hayo. Na wakati nilipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka mbele ya malaika aliyeyaonyesha kwangu kwa kumwabudu.


Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.


Nao walipoinua macho yao, hawakumwona mutu mwingine, isipokuwa Yesu peke yake.


Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.


Akaniambia: Danieli, wewe unayependwa sana, simama sawa usikilize kwa uangalifu maneno nitakayosema, maana nimetumwa kwako. Alipokuwa akiniambia maneno haya, mimi nilisimama nikitetemeka.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.


Mimi Danieli nilipoyaona maono hayo, na nilipokuwa nikijaribu kujua maana yake, kwa rafla, nikaona kiumbe kimoja chenye kufanana mwanadamu kikisimama mbele yangu.


Halafu mufalme Nebukadneza akaanguka uso mpaka chini na kumutukuza Danieli na kuamuru wamutolee Danieli sadaka na ubani.


Wewe mwanadamu, uelekeze uso wako kwenye milima ya Israeli, nawe utoe unabii kwa ajili ya wakaaji wake


Abramu akaanguka uso mpaka chini. Naye Mungu akamwambia:


Yule mutu akanipeleka mbele ya nyumba ya Yawe, kwa njia ya mulango wa kaskazini. Nilipoangalia, nikaona utukufu wa Yawe umeijaza nyumba ya Yawe. Hapo nikaanguka uso mpaka chini.


Nikajongea karibu na mutu mumoja kati ya wale waliosimama pale na kumwuliza maana kamili ya mambo hayo yote. Naye akanielezea maana yake akisema:


Mimi Danieli, nikazimia na kuugua kwa muda. Nilipopona, nikaendelea na shuguli za mufalme. Lakini yale maono yalishangaza, nami sikuweza kuyaelewa.


Naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Simama. Ninataka kusema nawe.


Halafu wafalme hao wawili wataikaa kwa meza pamoja, lakini kila mumoja anamuwazia mwenzake uovu, na kudanganyana. Lakini hawatafanikiwa, maana wakati uliopangwa utakuwa bado haujatimia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite