Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 8:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kisha, nikamusikia mutakatifu mumoja akizungumuza na mwenzake. Huyo mwenzake alimwuliza: Matukio ya mambo yaliyotangazwa katika maono haya yataendelea kwa muda gani? Kwa muda gani sadaka za kuteketezwa za kila siku zitaendelea kuzarauliwa? Kwa muda gani upotovu wa kuangamiza kila kitu utaendelea, na Pahali Patakatifu pamoja na viumbe vya mbingu vitaendelea kukanyagwa?

Gade chapit la Kopi




Danieli 8:13
38 Referans Kwoze  

Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Waaskari wake watalichafua hekalu na kuta zake, watakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku na kusimamisha kule katika hekalu chukizo linaloleta uharibifu.


Akili yake ya kimutu ibadilishwe, akuwe na akili ya nyama kwa miaka saba.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


“Wakati mutakapoona muji wa Yerusalema umezungukwa na waaskari, mujue kwamba uharibifu wake unakaribia.


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)


Sisi watakatifu wako tulirizi inchi kwa muda kidogo tu, lakini waadui zetu wakakuja wakaharibu hekalu lako.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?


Ni Enoki, mutu wa kizazi cha saba tangu Adamu, ndiye aliyetabiri zamani juu yao, akisema: “Musikilize, Bwana atakuja pamoja na maelfu na maelfu ya wamalaika zake watakatifu.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Tangu wakati wa kukomeshwa kwa sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, ni kusema kutoka wakati ule chukizo linaloleta uharibifu litakaposimamishwa, itakuwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi kenda.


Nilielezwa hivi: Yule nyama wa ine ni ufalme wa ine utakaokuwa katika dunia. Ufalme huo utakuwa tofauti na falme zingine, nao utaiangamiza dunia nzima. Utaiangusha chini na kuipasua vipandevipande.


Nikajongea karibu na mutu mumoja kati ya wale waliosimama pale na kumwuliza maana kamili ya mambo hayo yote. Naye akanielezea maana yake akisema:


Tena amri ile ya kukiacha kisiki na mizizi ya muti huo katika udongo ina maana hii: Wewe utarudishiwa tena ufalme wako wakati utakapotambua kwamba Mungu wa mbinguni ndiye anayetawala.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Hatuoni tena vitambulisho vya kuwa kwako kati yetu, hatuna tena nabii yeyote, wala hakuna anayejua mwisho wa haya yote!


Malaika wa Yawe akamujibu: “Kwa nini unataka kujua jina langu? Ni la ajabu.”


Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele?


Halafu agano lenu na kifo litavunjika, na mapatano yenu na kuzimu yatafutwa. Ile hasara kubwa itakapokuja itawaangusha chini.


Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu, wamekanyagakanyaga chini urizi wangu; shamba langu zuri wamelifanya jangwa.


Nilisikia lakini sikuelewa. Halafu, nikamwuliza: Bwana wangu, mwisho wa mambo haya yote utakuwa namna gani?


Nilipokuwa ninalala katika kitanda, niliona maono: Mulinzi mutakatifu alishuka kutoka mbinguni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite