Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Pembe dogo ile ikajitukuza mbele ya mukubwa wa viumbe vya mbinguni. Ikakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo mukubwa wa viumbe vya mbinguni alivyotambikiwa kila siku, na kuchafua hekalu lake.

Gade chapit la Kopi




Danieli 8:11
28 Referans Kwoze  

Tangu wakati wa kukomeshwa kwa sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, ni kusema kutoka wakati ule chukizo linaloleta uharibifu litakaposimamishwa, itakuwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi kenda.


Waaskari wake watalichafua hekalu na kuta zake, watakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku na kusimamisha kule katika hekalu chukizo linaloleta uharibifu.


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


Vilevile kila siku, sadaka ya kilo mbili za unga itatolewa asubui pamoja na litre moja ya mafuta ya muzeituni yakichanganywa na unga. Inafaa kufuata maagizo za sadaka hii kwa Yawe milele.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Viumbe vya mbinguni vikatiwa chini ya mamlaka yake pamoja na sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, kwa ajili ya upotovu. Nao ukweli ukatupwa chini. Pembe dogo ile ikaiangusha chini ibada ya kweli. Ilifanikiwa katika kila jambo iliyofanya.


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Wamoabu wataangamizwa, hata hawatakuwa tena taifa, kwa sababu walijitukuza mbele ya Yawe.


Mumuleweshe Moabu kwa sababu alijitukuza juu yangu mimi Yawe. Moabu atagaagaa katika matapiko yake na watu watamuchekelea.


Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.


Uwaambie kwamba sadaka watakayonitolea ya kuteketezwa kwa moto, itakuwa hii: wana-kondoo wawili wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema chochote, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


Atakuwa mwenye mamlaka makubwa, atasababisha uharibifu mubaya sana, na atafanikiwa katika kila atakalotenda. Atawaangamiza watu wenye uwezo na watakatifu wa Mungu.


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Makundi ya waaskari pamoja na kuhani wa hekalu wataangamizwa na kuwaua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite