Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 7:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.

Gade chapit la Kopi




Danieli 7:28
19 Referans Kwoze  

Basi Yesu akarudia Nazareti pamoja nao, akaendelea kuwatii. Na mama yake alichunga maneno haya yote katika moyo wake.


Lakini Maria akachunga mambo hayo yote ndani ya moyo na kuyafikiri sana.


Hivyo, niliachwa peke yangu nikiangalia hayo maono ya kushangaza. Nguvu zikaniishia, na uso wangu ukabadilika rangi, nikabaki bila nguvu.


Mimi Danieli, nikazimia na kuugua kwa muda. Nilipopona, nikaendelea na shuguli za mufalme. Lakini yale maono yalishangaza, nami sikuweza kuyaelewa.


Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika.


basi, ni wewe, ee mufalme, ambaye umekuwa mukubwa na mwenye nguvu. Ukubwa wako umefika mpaka mbinguni, na ufalme wako umeenea mpaka miisho ya dunia.


“Munitegee sikio vizuri: Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu.”


Mara moja, watu walipomwona Yesu, wakashangaa sana, wakakimbia kwenda kumusalimia.


Lakini wewe, ee Danieli, ujiendee, upumzike katika kaburi, na wakati huo utakapotimia, utafufuka na kupata zawadi yako.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Halafu wafalme hao wawili wataikaa kwa meza pamoja, lakini kila mumoja anamuwazia mwenzake uovu, na kudanganyana. Lakini hawatafanikiwa, maana wakati uliopangwa utakuwa bado haujatimia.


Kisha akaniambia: Sikiliza, ninakufahamisha jinsi matokeo ya kasirani ya Mungu yatakavyokuwa. Maono hayo yanaelekea wakati wa mwisho.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.


Lakini alipomwelezea baba yake na wandugu zake ndoto hiyo, baba yake alimukaripia, akisema: “Ni ndoto gani hiyo uliyoota? Itatupasa mimi, mama yako na wandugu zako kuja kuinama chini kwa heshima mbele yako?”


Wandugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akakuwa anafikiri juu ya jambo hilo.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Belsasari, mimi Danieli nikapata maono mengine zaidi ya maono yale ya kwanza.


Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.


Basi, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, akashangaa kwa muda, na mafikiri yake yakamufazaisha. Mufalme akamwambia: Beltesaza, ndoto hii, wala maana yake visikufazaishe! Beltesaza akamujibu: Bwana wangu, ingelikuwa heri ndoto hii na maana yake iwaelekee waadui zako!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite