Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 7:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.

Gade chapit la Kopi




Danieli 7:20
9 Referans Kwoze  

Nilielezwa hivi: Yule nyama wa ine ni ufalme wa ine utakaokuwa katika dunia. Ufalme huo utakuwa tofauti na falme zingine, nao utaiangamiza dunia nzima. Utaiangusha chini na kuipasua vipandevipande.


Nilipokuwa ninaziangalia hizo pembe, niliona pembe ingine ndogo ikiota katikati ya zile kumi, nayo ikaongoa pembe tatu kati ya hizo za kwanza. Pembe ile ilikuwa na macho ya kimutu na kinywa kilichosema maneno ya kujivuna.


Kutokana na maneno ya kujivuna yaliyokuwa yanasemwa na ile pembe, nikaendelea kuangalia. Nikaona yule nyama wa ine akiuawa, mwili wake ukaharibiwa na kutolewa uchomwe kwa moto.


Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba.


Kisha, katika maono hayo yangu ya usiku, nikaona nyama wa ine wa ajabu na wa kutisha, mwenye nguvu sana. Huyu alikuwa na meno makubwa ya chuma ambayo aliyatumia kwa kula na kuvunjavunja, na mabaki aliyakanyagakanyaga. Alikuwa tofauti na wale nyama wengine watatu, maana alikuwa na pembe kumi.


Kisha nikataka nielezwe juu ya yule nyama wa ine, ambaye alikuwa tofauti kabisa na wale wengine, wa kutisha sana, mwenye meno ya chuma na makucha ya shaba, aliyekula na kuvunjavunja, na kukanyagakanyaga yaliyobaki.


Nilipokuwa nikiangalia, pembe hio ilipigana vita na watakatifu, nayo ikawashinda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite