Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 6:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Danieli akamujibu mufalme: Uishi milele, ee mufalme!

Gade chapit la Kopi




Danieli 6:22
37 Referans Kwoze  

Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Petro alipotambua kwamba mambo yaliyotokea ni ya kweli akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Bwana alimutuma malaika wake kuniokoa katika mikono ya Herode na katika mabaya yote Wayuda waliotaka kunitendea.”


Kwa sababu hii ninajikaza siku zote kuishi maisha safi bila kuhukumiwa na zamiri yangu mbele ya Mungu na mbele ya watu.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.


Ninasikia watu wakinongonezana; kuna vitisho kila upande. Wanafanya shauri baya juu yangu, wanafanya mipango ya kuniua.


Yawe ambaye ameniokoa toka katika makucha ya simba na dubu, ataniokoa kutoka kwa Mufilistini huyu.” Saulo akamwambia: “Kwenda, naye Yawe akuwe pamoja nawe.”


Tukamulilia Yawe, naye akasikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri. Sasa tuko hapa Kadesi, muji unaopakana na inchi yako.


Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea


Mungu wangu alileta malaika wake kwa kufunga vinywa vya simba hawa, nao hawakunizuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina kosa lolote mbele yake na wala sijafanya jambo lolote baya mbele yako.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Wewe ni Mungu wangu, ninakushukuru; ninakutukuza, ee Mungu wangu.


Hao wanaonilipa mabaya kwa mazuri, wananipinga kwa sababu ninatenda mazuri.


Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia, na kumwokoa katika taabu zake zote.


Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimwita Mungu wangu. Toka katika hekalu lake alisikia sauti yangu; kilio changu kilifika katika masikio yake.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Ilipokuwa karibu saa tisa, Yesu akalalamika akisema: “Eli, Eli, lama sabaktani,” maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


Halafu akaendelea kusema: “Lakini kwa nini, wewe bwana wangu unanifuatilia mimi mutumishi wako? Nimefanya nini? Ni uovu gani nimekufanyia?


Maana mimi nilitoroshwa kutoka inchi ya Waebrania na hapa Misri sijafanya kitu chochote kinachostahili nitiwe katika kifungo.”


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Halafu Yeremia akamwuliza mufalme Zedekia: Nimekukosea nini, au nimewakosea nini watumishi wako au watu hawa, hata unitie katika kifungo?


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


Muzee akaenda, akaikuta maiti ya mutu wa Mungu katika barabara, simba na punda wake pembeni yake. Yule simba hakuikula maiti wala hakumushambulia punda.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite