Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.

Gade chapit la Kopi




Danieli 6:10
47 Referans Kwoze  

Lakini mimi ninamulilia Mungu, naye Yawe ataniokoa.


Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi alipojifanya mwenda-wazimu mbele ya mufalme Abimeleki naye akamufukuza na Daudi akajiendea.


Unawaangamiza wote wanaosema uongo; unawachukia wauaji na wadanganyifu.


Petro akawaamuru watu wote waende inje, akapiga magoti na kuomba. Kisha akaelekea ile maiti na kusema: “Tabita, simama!” Halafu Tabita akafungua macho, na wakati alipomwona Petro akaamuka na kuikaa.


Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari, maji mengi yakanizunguka, mawimbi na maji mengi vikapita juu yangu.


Solomono alipomaliza kusema maombi hayo yote na ombi lake kwa Yawe, alisimama kutoka pale mbele ya mazabahu ya Yawe, pahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu.


“Watu wako wakienda kwa vita kupigana na adui yao kwa upande wowote utakapowapeleka, nao wakikuomba wakielekea muji uliouchagua na nyumba niliyoijenga kwa ajili ya jina lako,


Kwa sababu hiyo ninapiga magoti mbele ya Baba Mungu,


Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba.


Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.


Paulo alipokwisha kusema maneno haya, akapiga magoti pamoja nao wote na kuomba.


Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”


tena kama watatubu kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote wakati watakapokuwa katika inchi ya uhamisho, na kama watakuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.


Lakini muda ule ulipotimia tukaondoka na kuendelea na safari yetu. Waamini wote pamoja na wanawake na watoto wao wakatusindikiza mpaka mbali na hata kufika kwenye kivuko cha muji. Kule sisi wote tukapiga magoti na kuomba.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


“Mwende ndani ya hekalu na mutangaze kwa watu maneno yote yanayoelekea uzima mupya.”


Na sasa Ee Bwana, angalia vitisho vyao. Basi utuwezeshe sisi watumishi wako tupate kutangaza neno lako kwa uhodari kabisa.


Siku moja, na saa tisa ya muchana, Petro na Yoane walienda katika hekalu kwa wakati wa maombi.


Watu hawa si walevi kama munavyozani, kwa sababu ingali tu saa tatu ya asubui.


Kisha akajitenga nao na kuenda kwenye hatua ya mutu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba akisema:


“Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile.


Wewe ni Mungu wangu; basi, unionee huruma, maana ninakulilia muchana kutwa.


Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,


Solomono alikuwa ametengeneza mimbari ya shaba ambayo aliweka katikati ya kiwanja. Urefu na upana wake ulikuwa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili na tano. Akapanda juu ya mimbari na kupiga magoti mbele ya watu wote wa Israeli, akainua mikono yake kuelekea mbinguni.


Usikilize wakati tunapokusihi, mimi mutumishi wako na watu wako Waisraeli ambao tutaomba tukielekea pahali hapa. Kutokea kwako mbinguni, usikilize. Na ukisha kusikiliza, utusamehe.


Nilimwomba Yawe, Mungu wangu, na kuitikia zambi, nikisema: Ee Bwana, wewe ni Mungu mukubwa na wa kuogopesha. Wewe unashika agano lako na kutenda mema kwa wanaokupenda na kuzitii amri zako.


Halafu Yesu akamwambia yule mwenye mukono unaokauka: “Simama hapa katikati.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite