Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 5:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.

Gade chapit la Kopi




Danieli 5:4
21 Referans Kwoze  

Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.


Basi kwa kuwa sisi tuko watoto wa Mungu, tusiwaze kwamba anafanana na sanamu ya zahabu au ya feza au ya jiwe, iliyochorwa kwa ufundi na akili ya watu.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Wote wanaotegemea sanamu za miungu, wote wanaoziambia “Ninyi ni miungu yetu” watakomeshwa na kupata haya.


Lakini Danieli aliamua kutojichafua kwa kula chakula bora cha mufalme na kunywa divai yake. Kwa hiyo, alimwomba yule mukubwa amuruhusu asikule vitu hivyo na kujichafua.


Basi, vile vyombo vya zahabu na feza vilivyokamatwa katika hekalu kule Yerusalema vikaletwa. Mufalme, wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake wakavitumia kwa kunywea.


Saa ileile, vidole vya mukono wa mwanadamu vikatokea na kuandika kwenye lipu ya ukuta wa nyumba ya kifalme uliopakaliwa chokaa pahali palipoangaziwa vizuri, mbele ya kinara cha taa. Mufalme aliuona mukono ule ukiandika.


Kwa hiyo mutakuwa wa kwanza kwenda katika uhamisho, na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.


Basi, waalikwa wa Adonia wakaogopa sana, wakaondoka na kutawanyika.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite