Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku moja mufalme Belsasari alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakubwa wake na kunywa divai pamoja nao.

Gade chapit la Kopi




Danieli 5:1
11 Referans Kwoze  

Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.


Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!


Wakiwa na hamu kubwa nitawatayarishia karamu: nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa siku zote na hawataamuka tena. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.


Upanga ukuwe juu ya Wakaldea, juu ya wakaaji wa Babeli na wakubwa na wenye hekima wake! –Ni ujumbe wa Yawe.–


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite