Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 4:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Nyuma ya miezi kumi na miwili, mufalme Nebukadneza alikuwa anatembea juu ya dari ya nyumba ya kifalme katika muji wa Babeli.

Gade chapit la Kopi




Danieli 4:26
13 Referans Kwoze  

Hii ndiyo ndoto niliyoota mimi Nebukadneza. Sasa, wewe Beltesaza, unielezee maana yake; maana wenye hekima wote katika ufalme wangu hawawezi kuniambia maana yake; lakini wewe utaweza kwa maana roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako.


Mwana wake akamwambia: ‘Baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile. Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako.’


Basi nitaondoka huku na kurudia kwa baba yangu nami nitamwambia: baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile.


Wanafunzi walipoona jambo hilo, wakashangaa sana na kujiuliza: “Namna gani muti huu umekauka mara moja?”


Lakini mimi ninawaambia: musiape hata kidogo kwa jina la mbingu, kwa maana ni kiti cha kifalme cha Mungu;


Tena amri ile ya kukiacha kisiki na mizizi ya muti huo katika udongo ina maana hii: Wewe utarudishiwa tena ufalme wako wakati utakapotambua kwamba Mungu wa mbinguni ndiye anayetawala.


Wewe, ee mufalme, mufalme wa wafalme! Mungu amekupa ufalme, uwezo, nguvu na utukufu!


Aliwaambia wamwombe Mungu wa mbinguni awaonee huruma juu ya fumbo hilo, kusudi wao wasiangamie pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.


Halafu Danieli akafunuliwa fumbo hilo usiku katika maono. Naye Danieli akamushukuru Mungu wa mbinguni,


Kwa mwisho wa ile miaka saba, mimi Nebukadneza niliinua macho yangu kuangalia juu mbinguni na akili zangu zikanirudilia. Nilimushukuru Mungu Mukubwa na kumuheshimu yeye anayeishi milele: Kwa sababu mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.


Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.


Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite