Danieli 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 basi, ni wewe, ee mufalme, ambaye umekuwa mukubwa na mwenye nguvu. Ukubwa wako umefika mpaka mbinguni, na ufalme wako umeenea mpaka miisho ya dunia.
Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.
Kwa sababu hiyo, ee mufalme, sikiliza shauri langu. Achana na zambi zako na maovu yako, utende haki na kuwaonea huruma walioteswa; labda muda wako wa kufanikiwa utarefushwa!
Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.
kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.
Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.
Daudi akamujibu: “Wewe si mwanaume? Nani anayekuwa sawa nawe katika Israeli? Mbona basi, haukumulinda bwana wako mufalme? Mutu mumoja kati yetu aliingia pale kwa kumwangamiza bwana wako mufalme!
Kwa maneno hayo, Daudi akawashawishi watu wake wasimuzuru Saulo; aliwakataza wasimushambulie. Kisha Saulo akasimama, akatoka ndani ya pango akaendelea na safari yake.
Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.
Akamwagiza yule aliyetangulia: “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza: ‘Wewe ni mutumishi wa nani? Unakwenda wapi? Na nyama hawa ni wa nani?’
Halafu Rakeli akamwambia baba yake: “Tafazali baba, usiuzike, maana siwezi kusimama mbele yako kwa sababu niko katika siku zangu.” Basi, Labani akatafuta sanamu za miungu yake, lakini hakuzipata.
Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.