Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 4:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Akili yake ya kimutu ibadilishwe, akuwe na akili ya nyama kwa miaka saba.

Gade chapit la Kopi




Danieli 4:13
18 Referans Kwoze  

Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.


Kisha, nikamusikia mutakatifu mumoja akizungumuza na mwenzake. Huyo mwenzake alimwuliza: Matukio ya mambo yaliyotangazwa katika maono haya yataendelea kwa muda gani? Kwa muda gani sadaka za kuteketezwa za kila siku zitaendelea kuzarauliwa? Kwa muda gani upotovu wa kuangamiza kila kitu utaendelea, na Pahali Patakatifu pamoja na viumbe vya mbingu vitaendelea kukanyagwa?


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:


Ni Enoki, mutu wa kizazi cha saba tangu Adamu, ndiye aliyetabiri zamani juu yao, akisema: “Musikilize, Bwana atakuja pamoja na maelfu na maelfu ya wamalaika zake watakatifu.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Tena amri ile ya kukiacha kisiki na mizizi ya muti huo katika udongo ina maana hii: Wewe utarudishiwa tena ufalme wako wakati utakapotambua kwamba Mungu wa mbinguni ndiye anayetawala.


Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:


Nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa nawe, ee Yawe? Nani anayekuwa sawa nawe kati ya miungu?


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


akisema: “Ee Yesu wa Nazareti, kuna maneno gani kati yako na sisi? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani. Wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


“Kuna maneno gani kati yako na sisi, wewe Yesu wa Nazareti? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani: wewe ni Mutakatifu aliyetumwa na Mungu.”


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


Nilielezwa hivi: Yule nyama wa ine ni ufalme wa ine utakaokuwa katika dunia. Ufalme huo utakuwa tofauti na falme zingine, nao utaiangamiza dunia nzima. Utaiangusha chini na kuipasua vipandevipande.


Nyama hao wane wakubwa ni wafalme wane watakaotokea katika dunia.


Nilipokuwa ninalala katika kitanda, niliona maono: Mulinzi mutakatifu alishuka kutoka mbinguni.


Mumusifu Yawe, enyi wamalaika wakubwa, enyi munaotimiza amri zake na kutimiza neno lake!


Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,


Anaondolea viongozi wa watu ujuzi wao, anawafanya watangetange katika jangwa kusikokuwa njia,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite