Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Wakati huo, watu wamoja kati ya Wakaldea wakajitokeza na kuwashitaki Wayuda. Walimwambia mufalme Nebukadneza:

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:8
14 Referans Kwoze  

Lakini tungependa kusikia mawazo yako kwa maana tunajua kwamba fasi zote watu wanapinga dini hii unayofuata.”


Wale Wakaldea wakamujibu: Mufalme, hakuna mutu yeyote katika dunia anayeweza kutimiza mapenzi yako. Hakuna mufalme yeyote, hata akuwe mukubwa na mwenye nguvu yapata gani aliyepata kuwauliza waganga au walozi au Wakaldea jambo kama hilo.


Tena alipogundua kwamba Mordekayi alikuwa Muyuda, akaamua kwamba kumwazibu peke yake haitoshi. Basi akafanya shauri la kuwaangamiza Wayuda wote, watu wa ukoo wa Mordekayi, katika utawala wa mufalme Ahasuero.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Basi, mufalme akaamuru waganga, walozi na wachawi wa Wakaldea waletwe kusudi wamufasirie ndoto yake. Wote wakakuja na kusimama mbele yake.


Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.


Nilipokuwa ninalala, niliona maono haya: Niliona muti murefu sana katikati ya dunia.


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite