Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Maliwali, wasimamizi, wakubwa wa majimbo na washauri wa mufalme, wote wakakusanyika pamoja, wakaona kwamba ule moto haukuweza kuwaunguza hao watatu. Nywele zao hazikuungua, nguo zao hazikuungua wala hawakuwa na harufu yoyote ya moto.

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:27
17 Referans Kwoze  

Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.


Basi ninawasihi ninyi mukule chakula, kwa sababu kitawafalia kusudi musikufe. Kwa maana hakuna mumoja kati yenu atakayepatwa na hasara yoyote hata kidogo.”


Na kwa upande wenu, yeye anajua hesabu ya nywele zote za vichwa vyenu.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe tu, ee Yawe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Basi, vijana hao wakafungwa wakiwa wamevaa makoti yao, kanzu zao, kofia na nguo zao zingine, wakatupwa katikati ya ile furu la moto mukali.


Mufalme Agripa anajua vizuri mambo yale yaliyotokea. Nami ninaweza kusema mbele yake pasipo woga kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna hata jambo kati ya hayo asilofahamu, kwa sababu hayakufanyika kwa uficho.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


Mungu wangu alileta malaika wake kwa kufunga vinywa vya simba hawa, nao hawakunizuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina kosa lolote mbele yake na wala sijafanya jambo lolote baya mbele yako.


Muzee akaenda, akaikuta maiti ya mutu wa Mungu katika barabara, simba na punda wake pembeni yake. Yule simba hakuikula maiti wala hakumushambulia punda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite