Danieli 3:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
25 Kisha akauliza: Lakini sasa mbona ninaona watu wane wakitembeatembea mule ndani ya moto bila kufungwa na wala hawaunguwi, na mutu wa ine anaonekana kama mwana wa miungu?
Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.
Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.
Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.
Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!
Basi, mufalme Nebukadneza akashangaa, akasimama kwa haraka na kuwauliza washauri wake: Si tuliwafunga watu watatu na kuwatupa katika moto? Nao wakamujibu mufalme: Kweli, mufalme! Ndivyo!
Mungu wangu alileta malaika wake kwa kufunga vinywa vya simba hawa, nao hawakunizuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina kosa lolote mbele yake na wala sijafanya jambo lolote baya mbele yako.