Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:19
26 Referans Kwoze  

Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.


basi, nami nitapingana nanyi na kuwaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Mwenye kiburi na majivuno jina lake ni “Mazarau”; anatenda kwa kujivuna tu.


basi nami nitapingana nanyi kwa hasira kali, na kuwaazibu mimi mwenyewe mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.


Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Kama mukiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, nitazidisha tena azabu yenu mara saba kadiri ya wingi wa zambi zenu.


Na kama hata kisha kuazibiwa hivyo hamutanisikiliza, basi, nitawaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Kwa hiyo mufalme akafurahi sana; akaamuru kwamba wamwondoe Danieli toka ndani ya pango. Basi wakamwondoa, naye hakuonekana na alama hata kidogo ya kidonda, kwa sababu alimutegemea Mungu wake.


Nami nitakitia katika mikono ya wanaokutesa, waliokuambia ulalie tumbo wapite juu yako, nawe ukaufanya mugongo wako kama vile udongo wa njia, kama vile barabara ya kupitia.


Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.


Mufalme akasimama kwa hasira, akatoka ndani ya chumba kwenye karamu ya divai na kwenda inje kwenye bustani ya nyumba ya kifalme. Hamani alipoona kwamba mufalme amekusudia kumwazibu, akabaki nyuma kwa kumusihi malkia Esteri ayaponyeshe maisha yake.


Yakobo alijua vilevile kwamba Labani hakumujali yeye kama pale mbele.


Kusikia hivyo, mufalme Nebukadneza alikasirika na kuwa na hasira sana, akaamuru wenye hekima wote wa Babeli waangamizwe.


Akaamuru watu fulani wenye nguvu kabisa kati ya waaskari wake wawafunge Sadiraki, Mesaki na Abedenego na kuwatupa katika ile furu ya moto mukali.


Hamani akawaka hasira alipojua kwamba Mordekayi hainami wala kupiga magoti mbele yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite