Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:15
25 Referans Kwoze  

Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme.


Ni nani kati ya miungu ya inchi hizi aliyeokoa inchi zao toka katika mikono yangu. Yawe ataweza kuukoa Yerusalema?’ ”


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Na mutakapokamatwa na kupelekwa kwa kuhukumiwa, musijihangaishe mbele ya wakati juu ya maneno mutakayosema, lakini museme maneno mutakayopewa saa ile ile. Kwa sababu hayatatoka kwenu wenyewe, lakini yatatoka kwa Roho Mutakatifu.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Na wote waliohuzuria katika lile Baraza wakamukazia Stefano macho, wakaona uso wake unafanana sawa na uso wa malaika.


Hivi utaweza labda kutoa matunda mwaka kesho! Kama si vile, basi utaukata!’ ”


“Wakati watakapowapeleka kwa kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia, au mbele ya watawala na ya wakubwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayojibu au yale mutakayosema,


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Lakini watakapowapeleka kwa kuhukumiwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayoyasema wala juu ya namna mutakavyosema, kwa maana saa ile ile mutapewa maneno mutakayoyasema.


kwamba musiponijulisha ndoto hiyo, azabu yenu ni moja. Mumepatana kunidanganyadanganya na kuniambia uongo kwa kungojea hali ibadilike. Muniambie ndoto hiyo, nami nitajua kwamba munaweza kunijulisha maana yake.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite