Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:13
15 Referans Kwoze  

Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


Kusikia hivyo, mufalme Nebukadneza alikasirika na kuwa na hasira sana, akaamuru wenye hekima wote wa Babeli waangamizwe.


Nyuma ya siku chache, liwali Feliki akakuja pamoja na muke wake Drusila, aliyekuwa Muyuda. Akaamuru wamwite Paulo, naye akasikiliza maneno aliyosema juu ya kumwamini Kristo Yesu.


Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,


Lakini wale wakubwa wakakasirika sana, wakaanza kusemezana wao kwa wao juu ya namna watakavyomutendea Yesu.


“Mujiangalie vizuri ninyi wenyewe, kwa maana watawapeleka mbele ya tribinali kwa kuwahukumu na kuwapiga fimbo katika nyumba za kuabudia. Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao.


Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao na mbele ya watu wa mataifa mengine.


Mwenye kasirani anachochea ugomvi, mutu wa hasira anasababisha makosa mengi.


Jiwe ni zito na muchanga vilevile, lakini uchokozi wa mupumbafu ni muzito zaidi.


Afazali kukutana na dubu dike aliyenyanganywa watoto wake, kuliko kukutana na mupumbafu katika upumbafu wake.


lakini hakupendezwa na Kaina wala na sadaka yake. Basi, Kaina akakasirika sana na uso wake ukakunjamana.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite