Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wewe, ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu anaposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na kila aina ya muziki, ainame chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu.

Gade chapit la Kopi




Danieli 3:10
24 Referans Kwoze  

Watu wale waliofanya mupango mubaya juu ya Danieli waliingia ndani, wakamukuta Danieli akiomba na kumusihi Mungu wake.


Nao wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mutu akijua pahali Yesu alipokuwa, alete habari kusudi wapate kumufunga.


Ninyi munapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi na kutunga ala mupya za muziki mukimwiga mufalme Daudi.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Ole kwao wanaotunga sheria za uovu, watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.


Zaidi ya hayo, nimegundua chini ya jua kwamba uovu unatawala kwa pahali pa haki na sheria.


Wewe hauwezi kushirikiana na waamuzi wapotovu, wanaotunga masharti za kutetea maovu.


Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika pamoja kwa shangwe kwa kubeba Sanduku la Agano la Yawe mpaka Yerusalema. Wakalisindikiza kwa mulio wa baragumu, ngunga, matoazi, na sauti kubwa za vinanda na vinubi.


Daudi aliwaamuru vilevile wakubwa wa Walawi wachague kati ya wandugu zao waimbaji wakuwe wanaimba na kupiga ala za muziki kwa nguvu, kwa kutoa sauti za furaha. Walipiga vinanda, vinubi na matoazi.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


“Munapofanya kazi ya kuzalisha wanawake Waebrania, ikiwa mutoto anayezaliwa ni mwanaume, mumwue. Ikiwa ni mwanamuke, mumwache aishi.”


Na kwamba mutu yeyote asiyeinama chini na kuiabudu sanamu hiyo, atupwe ndani ya furu la moto mukali.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite