Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 2:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.

Gade chapit la Kopi




Danieli 2:44
38 Referans Kwoze  

Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Ufalme wako ni ufalme wa milele; mamlaka yako yanadumu vizazi vyote. Yawe ni mwaminifu katika ahadi zake zote, ni mwema katika matendo yake yote.


Halafu mufalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na luga zote katika dunia: Ninawatakia amani kwa wingi.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamizwa; mataifa hayo yatateketezwa kabisa.


Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babeli waletwe mbele yangu kusudi wanielezee maana ya ndoto hiyo.


Wewe, ee mufalme, mufalme wa wafalme! Mungu amekupa ufalme, uwezo, nguvu na utukufu!


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Lakini, kuna Mungu mbinguni ambaye anafumbua mafumbo, naye amekujulisha, ee mufalme Nebukadneza, mambo yatakayotukia katika siku zinazokuja. Ndoto yako na maono yaliyokufikia ulipokuwa unalala ni haya:


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Atayatawala kwa fimbo ya chuma na kuyaponda kama vile mutungi,


Na lile kundi la watu wakamujibu: “Sisi tumesikia katika maandiko ya Sheria kwamba Kristo ataishi milele. Basi namna gani unaweza kusema kama Mwana wa Mutu anapaswa kunyanyuliwa juu? Na huyu Mwana wa Mutu ni nani?”


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


Ulipokuwa ukiangalia, jiwe liliongoka lenyewe, bila kuguswa, na kuipondaponda miguu ya shaba na udongo wa mufinyanzi ya ile sanamu, na kuivunja vipandevipande.


Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga,


Mara moja chuma, udongo wa mufinyanzi, shaba, feza na zahabu, vyote vikavunjika vipandevipande na vikakuwa kama maganda kwenye nafasi ya kupepetea ngano wakati wa jua. Upepo ukavipeperushia mbali wala hakukubakia hata kipande kimoja. Lakini lile jiwe lililoivunja ile sanamu likageuka kuwa mulima mukubwa na kuijaza dunia yote.


Hii ina maana kwamba watawala wa ufalme huo watachanganyikana kwa kuoana na watu wasiokuwa wa taifa lao, lakini hawatafikia kuchanganyikana kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mufinyanzi.


Nitayatikisa mataifa yote na mali zao zote zitaletwa humu, nami nitaifanya nyumba hii kuwa yenye utukufu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu na kiti chake cha kifalme cha ufalme wake nitakiimarisha milele.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Ninatoa amri katika ufalme wangu kwamba watu wote wanapaswa kumwogopa na kumuheshimu Mungu wa Danieli. Yeye ni Mungu Mwenye Uzima, anayeishi milele; ufalme wake hauwezi kuangamizwa hata kidogo, utawala wake hauna mwisho.


na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite