Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 2:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Lakini mimi sikufumbuliwa fumbo hili kwa sababu nina hekima kuliko wanadamu wengine, lakini kusudi wewe mufalme, upate kujulishwa maana ya ndoto yako na kujua mawazo yako.

Gade chapit la Kopi




Danieli 2:30
16 Referans Kwoze  

Yosefu akamujibu: “Sina uwezo ule; lakini Mungu atakupa jibu linalofaa.”


Petro alipoona maneno yale, akawaambia watu: “Wanainchi wenzangu Waisraeli, sababu gani munashangazwa na jambo hili? Sababu gani munatukazia macho? Munafikiri kwamba mutu huyu amepata kutembea kutokana na uwezo wetu sisi wenyewe au kwa haki yetu mbele ya Mungu?


Kwa maana mambo haya yote yanafika kwa ajili yenu kusudi neema ya Mungu izidishwe kwa watu wengi siku zote, nao wapate kumutolea Mungu shukrani nyingi kwa ajili ya utukufu wake.


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Na kama Bwana asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja ambaye angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya wachaguliwa aliowachagua amezipunguza.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!


Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Kwa ajili ya mutumishi wangu Yakobo, muchaguliwa wangu Israeli, nimekuita kwa jina lako; nimekupa jina la heshima ingawa wewe haunijui.


Nikiikaa au nikisimama, wewe unajua; wewe unajua kila kitu ninachofikiri juu yake.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite