Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wake, mufalme Nebukadneza aliota ndoto. Na kwa hiyo roho yake ikahuzunika sana hata hakuweza kupata usingizi.

Gade chapit la Kopi




Danieli 2:1
14 Referans Kwoze  

Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:


Usiku ule, mufalme hakupata usingizi. Basi, akaamuru kitabu cha Mambo ya Siku cha matukio ya kila siku, kiletwe, nacho kikasomwa mbele yake.


Mufalme Nebukadneza akawaambia: Niliota ndoto, nayo inanipa wasiwasi, nami ninataka nijulishwe maana yake.


Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Yoyakimu mwana wa Yosia, juu ya inchi ya Yuda, Yawe alimupa Yeremia ujumbe juu ya watu wa Yuda. Mwaka huo ulikuwa wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mufalme wa Babeli.


Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mulango wa lile pango. Mufalme akapiga muhuri wake mwenyewe na ule wa wakubwa wake, kusudi uamuzi uliotolewa juu ya Danieli usibadilishwe.


Basi, mufalme Belsasari akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakubwa wake wakakuwa na wasiwasi.


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:


Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.


Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite