Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 11:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Wamoja kati ya wenye hekima watauawa, kusudi wapate kuondolewa uchafu, kutakaswa na kusafishwa, mpaka wakati wa mwisho, ambao sasa bado haujatimia.

Gade chapit la Kopi




Danieli 11:35
34 Referans Kwoze  

Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali,


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Pembe dogo ile ilikomaa sana kufikia viumbe vya mbinguni; ikaangusha chini sehemu ya nyota na kuzikanyagakanyaga.


Tena ni yeye aliyewakulisha mana katika jangwa, chakula ambacho babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hayo yote kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kwa kuwapima apate kuwajalia mema kwa mwisho.


Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.


Malaika mwingine akatoka katika hekalu, akalalamika kwa sauti kubwa akimwambia yule aliyeikaa juu ya wingu: “Nyoosha kisu chako, uanze kuvuna, kwa maana dunia iko tayari kwa kuvunwa, nayo saa ya mavuno imetimia!”


Wanafunzi wengine wakamwambia: “Tumemwona Bwana.” Lakini Toma akawajibu: “Nisipoona alama za misumari katika mikono yake na kutia kidole changu katika kovu za misumari ile, nami nisipoingiza vidole vyangu ndani ya ubavu wake, sitaamini.”


Yeye anakata kila tawi linalokuwa ndani yangu lisilozaa matunda. Naye anasafisha kila tawi linalozaa matunda, kusudi lizae matunda mengi zaidi.


Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Wenye hekima kati ya watu watawafundisha wengi. Hata hivyo, kwa siku chache watauawa kwa upanga au kwa moto, watakamatwa mateka au kunyanganywa mali zao.


Katika wakati uliopangwa ataishambulia inchi ya kusini kwa mara ingine, lakini mara hii, mambo yatakuwa tofauti.


Halafu wafalme hao wawili wataikaa kwa meza pamoja, lakini kila mumoja anamuwazia mwenzake uovu, na kudanganyana. Lakini hawatafanikiwa, maana wakati uliopangwa utakuwa bado haujatimia.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Kisha akaniambia: Sikiliza, ninakufahamisha jinsi matokeo ya kasirani ya Mungu yatakavyokuwa. Maono hayo yanaelekea wakati wa mwisho.


Gabrieli akakuja karibu na pahali niliposimama. Mimi nikaogopa sana, hata nikaanguka uso mpaka chini. Lakini akaniambia: Wewe mutu, uelewe kwamba maono uliyoyaona yanaelekea wakati wa mwisho.


na hata wakati ambapo wajumbe wa wakubwa wa Babeli waliotumwa kwake kuuliza juu ya mambo ya ajabu yaliyotokea mule, Mungu, alimwacha ajiamulie mwenyewe, kusudi amupime na kujua yote yaliyokuwa ndani ya moyo wake.


Kisha Paulo na wenzake wakaingia ndani ya chombo, wakaondoka katika muji Pafo na kwenda katika muji Perga katika jimbo la Pamfilia. Walipofika kule Yoane aliyeitwa vilevile Marko akaachana nao na kurudi Yerusalema.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.


Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite