Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 11:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Waaskari wake watalichafua hekalu na kuta zake, watakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku na kusimamisha kule katika hekalu chukizo linaloleta uharibifu.

Gade chapit la Kopi




Danieli 11:31
18 Referans Kwoze  

Tangu wakati wa kukomeshwa kwa sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, ni kusema kutoka wakati ule chukizo linaloleta uharibifu litakaposimamishwa, itakuwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi kenda.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


“Zile pembe kumi ulizoona ni wafalme kumi, ambao hawajaanza bado kutawala, lakini watapewa mamlaka ya kutawala kama wafalme kwa muda wa saa moja pamoja na yule nyama.


“Wakati mutakapoona muji wa Yerusalema umezungukwa na waaskari, mujue kwamba uharibifu wake unakaribia.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


Atakuwa mwenye mamlaka makubwa, atasababisha uharibifu mubaya sana, na atafanikiwa katika kila atakalotenda. Atawaangamiza watu wenye uwezo na watakatifu wa Mungu.


Akawaambia: Muchafue nyumba ya Yawe kwa kuvijaza viwanja vyake maiti, kisha musonge mbele. Basi, wakaenda, wakawaua watu katika muji.


Yawe amechukia mazabahu yake na hekalu lake amelikataa. Amewaachilia waadui wazibomoe kuta za nyumba zake katika muji. Wakapiga kelele ndani ya nyumba ya Yawe kama kelele za wakati wa sikukuu.


Waadui wamenyoosha mikono yao, wapate kukamata vitu vyake vyote vya bei kali. Kweli umeona watu wa mataifa wakiingia ndani ya hekalu, watu ambao Yawe aliwakataza kuingia kati kusanyiko lake.


Watu wa Yuda wametenda maovu mbele yangu. Wameweka sanamu zenye kuchukiza ndani ya nyumba hii inayojulikana kwa jina langu na kuichafua.


Kwa maana watu wameniacha mimi na kuchafua nafasi hii kwa kufukizia miungu mingine ubani; miungu ambayo wao wenyewe, babu zao wala wafalme wa Yuda hawaijui. Zaidi ya ile wamejaza pahali hapa damu ya watu wasiokuwa na kosa,


Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite