Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 11:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Kwa uhodari mwingi, ataunda kundi kubwa la waaskari kusudi apate kuushambulia ufalme wa kusini, naye mufalme wa kusini atajibu mashambulizi hayo kwa kundi kubwa zaidi la waaskari na lenye nguvu sana. Lakini, mufalme wa kusini hatashinda kwa maana watafanya shauri baya juu yake.

Gade chapit la Kopi




Danieli 11:25
6 Referans Kwoze  

Sasa nitakuelezea ule ukweli wa mambo haya. Wafalme wengine watatu wataitawala inchi ya Persia. Hao watafuatwa na mufalme wa ine ambaye atakuwa tajiri kuliko wale waliomutangulia. Wakati atakapopata nguvu kwa ajili ya utajiri wake, ataanza kuushambulia ufalme wa Ugriki.


Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.


Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.


Wana wa mufalme wa kaskazini watakusanya kundi kubwa la waaskari na kujitayarisha kwa vita. Kundi hilo litasonga mbele kama mafuriko ya maji litapita na kupigana vita mpaka ndani ya muji wenye kuta wa waadui.


Mufalme wa kusini atakuwa mwenye nguvu. Lakini mumoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu kuliko yeye na utawala wake utakuwa mukubwa zaidi.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite