Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mwili wake ulingaa kama zabarajadi safi. Uso wake ulifanana na umeme, na macho yake yaliwaka kama ndimi za moto. Miguu na mikono yake ilingaa kama shaba iliyosafishwa sana. Sauti yake ilivuma kama sauti ya kundi kubwa la watu.

Gade chapit la Kopi




Danieli 10:6
18 Referans Kwoze  

Macho yake yalimetameta kama ndimi za moto, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji nyingi. Alikuwa na jina lililoandikwa juu yake, wala hakuna mutu aliyejua, isipokuwa yeye mwenyewe tu.


Na kule sura ya Yesu ikageuka wazi mbele yao. Uso wake ukangaa kama jua, nazo nguo zake zikametameta kama mwangaza.


Niliangalia, nikaona kulikuwa magurudumu mane, gurudumu moja pembeni ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama jiwe la zabarajadi.


Vilipokuwa vinakwenda, nilisikia sauti ya mabawa yao; sauti ya muvumo huo ilikuwa kama ile ya maji mengi, kama sauti ya ngurumo kutoka kwa Mungu wa majeshi, na kama kelele ya jeshi. Viliposimama, vilikunja mabawa yao.


Magurudumu hayo yalionekana kuwa ya namna moja, yanametameta kama jiwe la zabarajadi na umbo lao lilikuwa kama gurudumu ndani ya gurudumu lingine.


Viumbe vile vilikwenda na kurudia mbio kama vile umeme unavyoonekana.


wa tano wa mawe ya sadoniki, wa sita wa mawe ya akiki, wa saba wa mawe ya krisolite, wa nane wa mawe ya belulo, wa tisa wa mawe ya topazo, wa kumi wa mawe ya krisoparazo, wa kumi na moja wa mawe ya haikinto na wa kumi na mbili wa mawe ya amazito.


Kisha nikaona malaika mwingine mwenye uwezo akishuka toka mbinguni. Alikuwa akifunikwa na wingu, naye alikuwa na upindi wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingaa kama jua na miguu yake ilimetameta kama nguzo ya ndimi za moto.


Naye alipokuwa akiomba, sura yake ikageuka, nazo nguo zake zikageuka nyeupe sana na zenye kumetameta.


Miguu yao ilikuwa yenye kunyooka; upande wa chini wa miguu yao ulikuwa kama kwato za miguu ya mwana-ngombe, nazo zilimetameta kama shaba safi.


na mustari wa ine utakuwa wa zabarajadi, shohamu na yaspi. Yote yatatiwa kwenye kingo za zahabu.


Yeye aliangaa kama umeme na nguo yake ilikuwa nyeupe sana.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Tuatera hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa Mwana wa Mungu, anayekuwa na macho yanayometameta kama ndimi za moto, na miguu inayongaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana.


Mikono yake ni kama pete za zahabu, amevaa mawe ya bei kali. Kiwiliwili chake ni kama pembe za tembo zilizopambwa kwa mawe ya yakuti ya rangi ya samawi.


Basi, alinipeleka huko, nami nikamwona mutu aliyeonekana anaangaa kama shaba. Katika mikono yake mutu huyo alikuwa na kamba ya kitani ya kupima nayo pamoja na ufito wa kupima nao, naye alikuwa amesimama karibu na mulango.


Nilipoangalia, nikaona kitu kilichofanana na mwanadamu. Sehemu yake ya chini, iliyoonekana kama ndio kiuno chake, ilikuwa kama moto. Toka kiuno chake kwenda juu alimetameta kama vile shaba.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite