Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Danieli 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.

Gade chapit la Kopi




Danieli 10:12
26 Referans Kwoze  

Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.


Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,


Yule malaika akawaambia wale wanawake: “Musiogope, kwa maana ninajua ya kama munamutafuta Yesu aliyetundikwa juu ya musalaba.


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


Lakini Yesu akawaambia: “Kwa sababu gani munafazaika na kuwa na mashaka?


Siku hiyo ni siku ya mapumziko kamili nanyi mutafunga. Hili ni sharti la kufuata siku zote.


Hili ni sharti la kufuata siku zote: Siku ya kumi ya mwezi wa saba, ninyi wenyewe na hata wageni wanaoishi kati yenu, munapaswa kufunga kula siku hiyo na kuacha kufanya kazi.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


na kuniambia: ‘Paulo, usiogope! Sherti usambe mbele ya Mufalme wa Roma. Na tena kwa kuwa inamupendeza Mungu kukutendea mema, yeye ataokoa maisha ya watu hawa wote wanaosafiri pamoja nawe.’


Upendo wangu kwa ajili ya nyumba yako unanichoma. Matusi wanayokutukana yananiangukia.


Lakini malaika akawaambia: “Musiogope, kwa sababu ninawaletea Habari Njema itakayofurahisha sana watu wote.


Halafu malaika akamwambia: “Maria, usiogope, kwa maana Mungu amekujalia neema.


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.


Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”


Akaniambia: Danieli, wewe unayependwa sana, simama sawa usikilize kwa uangalifu maneno nitakayosema, maana nimetumwa kwako. Alipokuwa akiniambia maneno haya, mimi nilisimama nikitetemeka.


Siku ya kumi ya mwezi wa saba mutafanya mukutano mutakatifu. Siku hiyo munapaswa kufunga kula na musifanye kazi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite