Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.

Gade chapit la Kopi




Amosi 9:7
14 Referans Kwoze  

Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote, kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona. Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini, watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.


Tigilati-Pileseri, akiitika kwa ombi la Ahazi, aliushambulia muji wa Damasiki na kuuteka. Akamwua mufalme Resini na kuwapeleka wafungwa kule Kiri.


Waavi walikuwa zamani wakiishi katika vijiji vya kando ya Mediteranea mpaka Gaza. Wakafutori kutoka kisiwa cha Kafutori wakawaangamiza, wakaishi humo pahali pao.)


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki, na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni, pamoja na mutawala wa Beti-Edeni. Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.


Mwetiopia anaweza kubadilisha rangi yake, au chui madoadoa yake? Nanyi muliozoea kufanya mabaya, munaweza namna gani kutenda mema?


Majeshi ya Elamu, pinde na mishale katika mikono, walikuja wamepanda farasi na magari ya vita; nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.


Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Asa alitoka akaenda kupigana naye. Pande zote mbili zilijipanga katika Bonde la Sefata karibu na Maresa.


Asa pamoja na waaskari wake wakawafuatilia mpaka Gerari, wakawaua Waetiopia wengi sana, hapakubaki hata mumoja, maana walikuwa wamekwisha kushindwa na Yawe pamoja na jeshi lake. Jeshi la Yuda likateka vitu vingi sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite