Amosi 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Hata wakijificha juu ya mulima Karmeli, huko nitawatafuta na kuwakamata; hata wakijificha mbali nami katika vilindi vya bahari, mule nitaiamuru nyoka kubwa ya bahari iwaume.
Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.
Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.
Amosi alisema hivi: Yawe ananguruma toka mulima Sayuni, anavumisha sauti yake toka Yerusalema, hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka, majani ya mulima Karmeli yananyauka.