Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 9:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.

Gade chapit la Kopi




Amosi 9:11
37 Referans Kwoze  

Kisha utawala wa wema utazinduliwa katika hema ya Daudi. Mutawala atakuwa mwaminifu. Atahukumu kufuatana na sheria ya Mungu, atakuwa mwepesi wa kutenda kwa haki.


Matawi yake yalienea mpaka kwa bahari; navyo vichipukizi vyake mpaka kando ya muto Furati.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Nitawafanya watu na nyama waongezeke na kuwa wengi. Nitawafanya ninyi milima mukaliwe tena kama zamani. Nitawatendea mema mengi kuliko zamani. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Halafu miti yote katika inchi itajua kwamba mimi Yawe ninaishusha miti mirefu na kuinua miti mifupi. Mimi ninakausha miti mibichi na kustawisha miti yenye kukauka. Ni mimi Yawe ninayesema hayo na nitayafanya.


Utugeuze, ee Yawe, kusudi tukurudilie. Uturudishie hali ya zamani.


Nitawatia katika mikono ya wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao, ni kusema Nebukadneza mufalme wa Babeli na wakubwa wake. Kisha, inchi ya Misri itakaliwa na watu kama ilivyokuwa hapo zamani. –Ni ujumbe wa Yawe.


Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.


Si wewe mwenyewe unamulinda pande zote pamoja na jamaa yake na kila kitu anachokuwa nacho? Wewe umemubariki na mali yake imeongezeka katika inchi.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Nao hawatakuwa tena watumwa wa wageni, lakini watanitumikia mimi Yawe, Mungu wao pamoja na mufalme wa ukoo wa Daudi ambaye nitakayewasimikia.


Ninakumbuka siku za zamani, ninafikiri juu ya yote uliyotenda, ninawazawaza matendo yako.


Umefuta agano ulilofanya na mutumishi wako; umeitupa taji yake ya kifalme ndani ya mavumbi.


Edomu itakuwa urizi wake, Seiri itakuwa mali yake, Israeli itapata ushindi mukubwa.


Watu wako watajenga tena mabomoko ya zamani; mutajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani. Nanyi mutaitwa watu waliotengeneza upya kuta, watu waliotengeneza tena barabara za miji.


Nitawajalia watu wa Yakobo, na Yuda nitamujalia watakaorizi milima yangu; wachaguliwa wangu watairizi, watumishi wangu watakaa kule.


Vilevile inaweza kunifikia kukusudia wakati wowote juu ya taifa au ufalme fulani kwamba nitalijenga na kulistawisha.


Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni nao utakuwa mulima mutakatifu. Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.


Usifurahie hali yangu ewe adui yangu! Nikianguka, nitasimama tena; nikiwa katika giza, Yawe ni mwangaza wangu.


Siku inakuja ambapo kuta za muji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya inchi yenu itapanuliwa.


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Nami Yawe nitasaidia kwanza jamaa za Yuda kusudi wazao wa Daudi na wakaaji wa Yerusalema wasijione kuwa wenye utukufu zaidi kuliko watu wengine wa kabila la Yuda.


Inchi yote, tangu Geba mpaka Rimoni, upande wa kusini wa Yerusalema, itageuzwa kuwa mbuga yenye kunyooka kabisa. Lakini Yerusalema utabaki juu pahali pake tokea mulango wa Benjamina mpaka kwenye mulango wa zamani, hata kwenye mulango wa Konani, tangu munara wa Hanameli mpaka kwenye kikamulio cha mufalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite