Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.

Gade chapit la Kopi




Amosi 9:1
28 Referans Kwoze  

Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa; Bwana wetu Yawe pekee ndiye anayeokoa katika kifo.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako, kumwokoa yule uliyemusimika kwa kumupakaa mafuta. Ulimuponda mutawala wa jamii ya waovu, ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,


Yoane akatoa ushuhuda huu: “Nimemwona Roho akishuka juu yake toka mbinguni kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Makundi ya nyama wa kufugwa watalala ndani yake, vilevile kila nyama wa pori. Tai, nyangenyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake, bundi watalia kwenye madirisha yake, vibombobombo watalia kwenye vizingiti, maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.


Utukufu wa Yawe ukapanda juu tokea wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha nyumba hiyo, na lile wingu likaijaza nyumba, na kiwanja kilijaa mwangaza wa utukufu wa Yawe.


Watu sita wakakuja kutoka upande wa mulango wa juu unaoelekea upande wa kaskazini, kila mumoja na silaha yake ya kuangamiza katika mukono wake. Pamoja nao, kulikuwa mutu mumoja ambaye alikuwa amevaa nguo ya kitani, naye ana chupa la wino. Wakaingia ndani ya hekalu, wakasimama pembeni ya mazabahu ya shaba.


Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.


Atakayetoroka kitisho atatumbukia ndani ya shimo; atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Kwa maana nitaleta mambo hayo juu ya Moabu, katika mwaka wao wa azabu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


Kisha Mikaya akasema: “Basi sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akikaa katika kiti chake cha kifalme na jeshi lake lote la mbinguni likisimama upande wake wa kuume na wa kushoto.


Ee mufalme, nilipokuwa katika njia, ilipotimia saa sita ya muchana, nikaona mwangaza unaotoka mbinguni unaopita mwangaza wa jua. Mwangaza ule ukanizunguka pamoja na wenzangu waliosafiri nami.


Kisha malaika mwingine akakuja kusimama karibu na mazabahu. Alikuwa akishika chetezo cha zahabu. Naye akapewa ubani mwingi kusudi autoe sadaka pamoja na maombi ya watu wote wa Mungu juu ya mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya kiti cha kifalme.


Mungu ataviponda vichwa vya waadui zake, ndivyo vichwa vya wanaoendelea katika njia mbaya.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Nitaleta hasara juu yao ambayo hawataweza kuiepuka. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza.


basi, vita munavyoviogopa vitawakuta kulekule Misri, na njaa munayoogopa itawaandama vikali mpaka Misri, na mutakufia kulekule.


Nitawaazibu vikali. Hata kama wataukimbia moto, huo moto utawateketeza. Hapo nitakapowaazibu vikali, halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.


Yoshua akasema: “Muviringishe mawe makubwa kwenye mulango wa pango na kuweka walinzi pale.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite