Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Siku zinakuja ambapo nitaleta njaa katika inchi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini si njaa ya kukosa chakula wala kiu ya kukosa maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Yawe.

Gade chapit la Kopi




Amosi 8:11
12 Referans Kwoze  

Hatuoni tena vitambulisho vya kuwa kwako kati yetu, hatuna tena nabii yeyote, wala hakuna anayejua mwisho wa haya yote!


Wakati huo, kijana Samweli alipokuwa anamutumikia Yawe chini ya uangalizi wa Eli, ujumbe kutoka kwa Yawe ulikuwa mara haba tu; hata na maono kutoka kwake yalipatikana mara chache.


Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.


Hata alipomwomba Yawe shauri, Yawe hakumujibu kwa ndoto, kwa mawe ya kupiga kura, wala kwa njia ya manabii.


Watapata hasara kwa mufululizo; nazo habari mbaya zitafuatana. Watamwomba nabii awatabirie. Makuhani hawatakuwa na sheria yoyote; na wazee watakosa shauri la kuwapatia.


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono, kutakuwa giza kwenu bila ufunuo. Jua litatua juu yenu, na muchana utakuwa giza kwenu.


Samweli akamwambia Saulo: “Kwa nini unanisumbua kwa kunipandisha?” Saulo akamujibu: “Mimi nina taabu kubwa! Wafilistini wananishambulia kwa vita, na Mungu ameniachilia. Hanijibu tena kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Ndiyo maana nimekuita unijulishe kitu cha kufanya.”


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.


Basi, muwaite wakaka zenu, “Watu wangu”, na wadada zenu, “Waliohurumiwa”.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite