Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Niliwaona nzige hao wakikula na kumaliza kila jani katika inchi. Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi utuhurumie! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!

Gade chapit la Kopi




Amosi 7:2
20 Referans Kwoze  

Nilipokuwa ninatabiri, Pelatia mwana wa Benaya akakufa. Nami nikaanguka uso mpaka chini, nikalia kwa sauti kubwa, nikisema: Ee Bwana Yawe, utawamaliza kabisa Waisraeli waliobaki?


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Wakati walipokuwa wakiwaua, mimi niliachwa peke yangu, nikaanguka uso mpaka chini, nikalia: Ee Bwana wangu Yawe, utaangamiza watu wote wa Israeli waliobaki, ukitimiza kasirani yako juu ya Yerusalema?


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Walifunika inchi yote ya Misri, hata inchi ikaonekana kuwa giza. Walikula mimea yote na matunda yote yaliyobaki wakati wa ile mvua ya mawe. Hakuna hata jani moja lililobakia katika inchi. Hakuna jani lolote lililobakia juu ya miti wala mimea popote katika inchi yote ya Misri.


Wakaambiwa wasiharibu majani yoyote wala mumea wowote, wala muti wowote, lakini wawatese watu wasiokuwa na chapa ya muhuri wa Mungu kwenye paji za nyuso zao.


Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi uache kuazibu! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!


Ee Yawe, utusikie; utusamehe ee Yawe. Ee Yawe, kwa ajili ya heshima yako utusikie na utende, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya muji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!


Hasara hizi mbili zimekupata: uharibifu na maangamizi; njaa na mauaji. Nani atakayekuonea huruma? Nani atakayekufariji?


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.


Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.


Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?


Niliwapiga pigo la ukosefu wa maji na ukungu; nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu; nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite