Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Usitoe tena unabii hapa katika Beteli, kwa sababu hapa ni pahali ya ibada ya mufalme; ni hekalu la utawala huu.

Gade chapit la Kopi




Amosi 7:13
14 Referans Kwoze  

Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai, na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.


Yeroboamu aliamuru vilevile siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane ikuwe sikukuu sawa na ile sikukuu iliyokuwa inafanyika kule Yuda. Alitoa sadaka kwenye mazabahu aliyotengeneza kule Beteli mbele ya zile sanamu za wana-ngombe alizozitengeneza, akaweka wale makuhani aliowachagua watumike kila nafasi ya kutolea sadaka aliyotengeneza juu ya vilima.


Akaiweka sanamu moja katika muji wa Beteli, na ya pili katika muji wa Dani.


Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Wajumbe wa baraza wakakubali shauri la Gamalieli. Halafu wakawaita mitume, wakawapiga fimbo na kuamuru wasifundishe tena kwa jina la Yesu. Kisha wakawaacha kwenda.


akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”


Wanawaambia wale wanaopata maono hivi: Musipate maono. Wanawaambia manabii hivi: Musitutangazie ukweli, lakini mutuambie mambo ya kupendeza, mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Nawe basi, ewe Amazia, sikiliza neno la Yawe: Wewe unaniambia nisitoe unabii juu ya Waisraeli, wala nisiseme neno lolote juu ya wazao wa Isaka.


Alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zile zambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Kwa nini umetabiri kwa jina la Yawe, ukisema kwamba nyumba hii itaharibiwa kama ile ya Shilo na muji huu utakuwa ukiwa, bila wakaaji? Na watu wote wakamuzunguka Yeremia katika nyumba ya Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite