Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kisha Amazia akamwambia Amosi: Sasa tumechoka nawe, ewe nabii! Uende! Urudie katika inchi ya Yuda, utoe unabii kule upate na chakula chako kulekule.

Gade chapit la Kopi




Amosi 7:12
16 Referans Kwoze  

Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Basi watu wote wa muji wakatoka kwa kumufikia Yesu na wakati walipomwona wakamusihi aondoke katika inchi yao.


(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Basi wakakuja, wakawabembeleza, wakawapeleka inje ya kifungo na kuwasihi watoke katika muji ule.


Kwa saa zile Wafarisayo wamoja walimwendea Yesu na kumwambia: “Ondoka hapa uende fasi ingine, maana mufalme Herode anataka kukuua.”


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai, na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.


Mumenizaraulisha mbele ya watu wangu kusudi mupate vitanga vya shayiri na chakula kidogo. Munawaua watu wasiostahili kufa na kuwaacha wazima wanaostahili kuuawa, kwa uongo wenu munaowaambia watu wangu, nao wanawaaminia.


Hao ni kama imbwa walafi sana, wala hawawezi kutosheka hata kidogo. Wachungaji nao hawana akili yoyote. Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe, kila mumoja anatafuta faida yake.


Wanawaambia wale wanaopata maono hivi: Musipate maono. Wanawaambia manabii hivi: Musitutangazie ukweli, lakini mutuambie mambo ya kupendeza, mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.


Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.


Yeyote atakayebakia katika jamaa yako atamwendea kuhani yule na kumwomba kikoroti cha feza au mukate, na kumwambia: Ninakuomba uniweke kwenye nafasi moja ya kuhani kusudi niweze kupata tu kipande cha mukate.”


Anachosema ni hiki: Yeroboamu atakufa kwa upanga nao Waisraeli watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite