Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo na kujinyoosha juu ya matandiko yao, mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!

Gade chapit la Kopi




Amosi 6:4
18 Referans Kwoze  

Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa.


Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.


Mazarau yanatokana na unene wao; mioyo yao inatiririka mipango mibaya.


Pahali pale kulikuwa kumepambwa kwa mapazia ya pamba ya rangi nyeupe na vitambaa vya rangi ya samawi. Mapazia hayo yalikuwa yamefungiwa pete za feza kwa kamba za kitani safi nyekundu-nyeusi, na kutundikwa kwenye nguzo za mawe ya marimari. Viti vya zahabu na feza vilikuwa vimewekwa kwenye sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi ya marimari, nyekundu, nyeusi, manjano na nyeusi.


Usiingie katika nyumba watu wanamofanya karamu. Usiikae kula na kunywa pamoja nao.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Kisha wakaikaa kwenye vitanda vizurivizuri, na mbele yao meza imetandikwa. Juu ya meza hiyo uliweka ubani wangu na mafuta yangu.


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Walipoikaa kwa kula wakainua macho na kuona kundi la Waisimaeli wakisafiri kutoka Gileadi kwenda Misri. Ngamia wao walikuwa wakibeba ubani, zeri na manemane.


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite