Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.

Gade chapit la Kopi




Amosi 6:12
17 Referans Kwoze  

Angalisho, enyi munaogeuza sheria kuwa uchungu, na kuona haki kuwa kama takataka!


Wanachosema ni maneno matupu; wanaapa na kufanya mapatano ya bure; haki imekuwa si haki tena, inachipuka kama mimea yenye sumu katika shamba.


Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu; kichwa kigumu kama chuma, uso wako kama shaba.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Lakini ninyi mumepanda uovu, ninyi mumevuna ubaya; mumekula matunda ya uongo wenu. Wewe Israeli ulitegemea nguvu zako mwenyewe, na wingi wa waaskari wako.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Na tunda la haki linapandwa katika amani na wale wanaopenda amani.


Nitamwua mutawala wa Moabu, pamoja na waongozi wote wa inchi hiyo. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite